Skip to content
July 11, 2026
  • Facebook
  • Twitter
  • Linkedin
  • Youtube
  • Instagram
Bunda FM

Bunda FM

Ngurumo ya jamii

Connect with Us

  • Facebook
  • Twitter
  • Linkedin
  • Youtube
  • Instagram

Tags

Afya Burudani Kimataifa Kitaifa Makala Michezo Muziki Siasa Uchumi na Biashara

Categories

  • Afya
  • Burudani
  • Kimataifa
  • Kitaifa
  • Makala
  • Michezo
  • Muziki
  • Siasa
  • Uchumi na Biashara
  • Home
  • Habari Zote
  • Kitaifa
  • Kimataifa
  • Michezo
  • Siasa
  • Uchumi na Biashara
  • About us
  • Contact
STAFF LOGIN
  • Home
  • Tume Ya Utawala Bora Yaing’ang’ania Polisi
  • Kitaifa
  • Siasa

Tume Ya Utawala Bora Yaing’ang’ania Polisi

gasper June 7, 2022 1 min read

Wakati kukiwa na malalamiko ya wananchi dhidi ya Jeshi la Polisi kudaiwa kuhusika katika mauaji ya watuhumiwa wanaokamatwa, Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB), imeingilia kati suala hilo na kupendekeza makosa yote ya jinai yanayowahusu askari polisi yachunguzwe na taasisi nyingine huru za umma.

Tume hiyo imelitaka pia Jeshi la Polisi lihakikishe utendaji wake wa kazi unazingatia sheria, kanuni na miongozo ya utekelezaji wa majukumu ya jeshi hilo.

Walipotafutwa kuzungumzia mapendekezo hayo ya tume, Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Simon Sirro na msemaji wa jeshi hilo, David Misime hawakupatikana mara moja, licha ya jitihada za kuwapigia simu na kuwatumia ujumbe mfupi.

Hata hivyo, Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamad Masauni alisema aliunda timu maalumu kuchunguza malalamiko aliyoyapokea ya mauaji yanayofanywa na polisi na tayari imemkabidhi ripoti kwa ajili ya utekelezaji.

“Nataka nikupe tu taarifa kwamba mimi nilishaunda hiyo timu na imefanya hiyo kazi ya kuchunguza malalamiko ambayo niliyapata kama waziri au niliyosikia kupitia vyombo vya habari na ile timu ilihusisha watu kutoka taasisi mbalimbali, na tayari imeniletea ripoti yake na nimeshaanza kuifanyia kazi,” alisema Masauni.

Waziri huyo aliongeza kwamba Jumatatu ijayo, atakutana na uongozi wa Jeshi la Polisi nchini ukiongozwa na IGP Sirro na timu yake ili kujadiliana haya matukio ambayo yamejitokeza hivi karibuni ambayo hayakuwepo kwenye ripoti ya tume yake.

gasper

See author's posts

Continue Reading

Previous: Simba Yaleta Mchezaji Mpya
Next: Waziri Mkuu Aitaka Tamisemi Isimamie Ukusanyaji Mapato

Habari nyingine

Kesi ya Sabaya yaahirishwa tena
1 min read
  • Kitaifa

Kesi ya Sabaya yaahirishwa tena

June 20, 2022
Sababu risiti za EFD kufutika maandishi yatajwa
1 min read
  • Kitaifa

Sababu risiti za EFD kufutika maandishi yatajwa

June 20, 2022
Mapacha Wenye Miaka 9 Mkoani Arusha Wanaishi Kwa Kula Magodoro
1 min read
  • Afya
  • Kitaifa
  • Makala

Mapacha Wenye Miaka 9 Mkoani Arusha Wanaishi Kwa Kula Magodoro

June 7, 2022

RATIBA YA VIPINDI VYETU

  • 05:00-06:00:- Hamka na Bunda FM
  • 06:00-07:00:- Habari za Ulimwengu (DW)
  • 07:00-07:10:- Taarifa ya Habari
  • 07:10-08:00:- Gospel Saturday
  • 08:00-09:00:- Matukio ya Week
  • 09:00-11:00:- Bahari ya Watoto
  • 11:00-13:00:- Orojo wa Pwani
  • 13:00-14:00:- Habari za Ulimwengu (DW)
  • 14:00-16:00:- Maabara ya Vijana
  • 16:00-18:00:- Asili Yetu
  • 18:00-19:00:- Habari za Ulimwengu (DW)
  • 19:00-19:10:- Taarifa ya Habari
  • 19:10-20:00:- Shamba Darasa
  • 20:00-21:00:- Flavor 921
  • 21:00-22:00:- B-Sport
  • 22:00-01:00:- Shangwe la Weekend
  • 01:00-05:00:- Usiku Mnene

  • Afya (2)
  • Burudani (4)
  • Kimataifa (4)
  • Kitaifa (9)
  • Makala (4)
  • Michezo (2)
  • Muziki (1)
  • Siasa (1)
  • Uchumi na Biashara (1)

Wasiliana nasi

Bunda FM LTD, 92.1 MHz
P.O. BOX 452
BUNDA-MARA
E-mail: Ngurumoyajamii@bundafm.co.tz
PNONE NO: +255 754 279 340
+255 755 029 400
+255 717 457 216

Masafa yetu

Our major frequency is 92.1 FM, whereby we cover regions of Mara, Simiyu, Mwanza, Geita,Kagera, Shinyanga, Singida, Tabora and Katavi regions.

  • Home
  • Habari Zote
  • Kitaifa
  • Kimataifa
  • Michezo
  • Siasa
  • Uchumi na Biashara
  • About us
  • Contact
Copyright © All rights reserved. | DarkNews by AF themes.