Skip to content
March 20, 2023
  • Facebook
  • Twitter
  • Linkedin
  • Youtube
  • Instagram
Bunda FM

Bunda FM

Ngurumo ya jamii

Connect with Us

  • Facebook
  • Twitter
  • Linkedin
  • Youtube
  • Instagram

Tags

Afya Burudani Kimataifa Kitaifa Makala Michezo Muziki Siasa Uchumi na Biashara

Categories

  • Afya
  • Burudani
  • Kimataifa
  • Kitaifa
  • Makala
  • Michezo
  • Muziki
  • Siasa
  • Uchumi na Biashara
  • Home
  • Habari Zote
  • Kitaifa
  • Kimataifa
  • Michezo
  • Siasa
  • Uchumi na Biashara
  • About us
  • Contact
STAFF LOGIN
  • Home
  • Tume Ya Utawala Bora Yaing’ang’ania Polisi
  • Kitaifa
  • Siasa

Tume Ya Utawala Bora Yaing’ang’ania Polisi

gasper June 7, 2022 1 min read

Wakati kukiwa na malalamiko ya wananchi dhidi ya Jeshi la Polisi kudaiwa kuhusika katika mauaji ya watuhumiwa wanaokamatwa, Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB), imeingilia kati suala hilo na kupendekeza makosa yote ya jinai yanayowahusu askari polisi yachunguzwe na taasisi nyingine huru za umma.

Tume hiyo imelitaka pia Jeshi la Polisi lihakikishe utendaji wake wa kazi unazingatia sheria, kanuni na miongozo ya utekelezaji wa majukumu ya jeshi hilo.

Walipotafutwa kuzungumzia mapendekezo hayo ya tume, Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Simon Sirro na msemaji wa jeshi hilo, David Misime hawakupatikana mara moja, licha ya jitihada za kuwapigia simu na kuwatumia ujumbe mfupi.

Hata hivyo, Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamad Masauni alisema aliunda timu maalumu kuchunguza malalamiko aliyoyapokea ya mauaji yanayofanywa na polisi na tayari imemkabidhi ripoti kwa ajili ya utekelezaji.

“Nataka nikupe tu taarifa kwamba mimi nilishaunda hiyo timu na imefanya hiyo kazi ya kuchunguza malalamiko ambayo niliyapata kama waziri au niliyosikia kupitia vyombo vya habari na ile timu ilihusisha watu kutoka taasisi mbalimbali, na tayari imeniletea ripoti yake na nimeshaanza kuifanyia kazi,” alisema Masauni.

Waziri huyo aliongeza kwamba Jumatatu ijayo, atakutana na uongozi wa Jeshi la Polisi nchini ukiongozwa na IGP Sirro na timu yake ili kujadiliana haya matukio ambayo yamejitokeza hivi karibuni ambayo hayakuwepo kwenye ripoti ya tume yake.

gasper

See author's posts

Continue Reading

Previous: Simba Yaleta Mchezaji Mpya
Next: Waziri Mkuu Aitaka Tamisemi Isimamie Ukusanyaji Mapato

Habari nyingine

1 min read
  • Kimataifa
  • Kitaifa

March 12, 2023
NECTA Yasitisha Kutangaza Shule Bora na Mwanafunzi Bora
1 min read
  • Kitaifa

NECTA Yasitisha Kutangaza Shule Bora na Mwanafunzi Bora

January 29, 2023
Matokeo kidato cha nne 2022 yatangazwa, haya hapa
1 min read
  • Kitaifa

Matokeo kidato cha nne 2022 yatangazwa, haya hapa

January 29, 2023

RATIBA YA VIPINDI VYETU

  • 05:00 - 06:00 :- Hamka na Bunda FM
  • 06:00-06:30:- Habari za Ulimwengu (DW)
  • 06:30-07:00:- Ukurasa Mpya
  • 07:00-07:10:- Taarifa ya Habari
  • 07:10-10:00:- Ukurasa Mpya
  • 10:00-13:00:- Mchaka Mchaka
  • 13:00-14:00:- Habari za Ulimwengu (DW)
  • 14:00-16:00:- Ladha Kamili
  • 16:00-18:00:- Busati la Habari
  • 18:00-18:30:- Habari za Ulimwengu (DW)
  • 18:30-19:00:- Dance Africa
  • 19:00-19:10:- Taarifa ya Habari
  • 19:10-21:00:- Dance Africa
  • 21:00-22:00:- B-Sport
  • 22:00-01:00:- Planet Love
  • 01:00-04:00:- Usiku Mnene

  • Afya (2)
  • Burudani (5)
  • Kimataifa (6)
  • Kitaifa (16)
  • Makala (4)
  • Michezo (4)
  • Muziki (1)
  • Siasa (3)
  • Uchumi na Biashara (1)

Wasiliana nasi

Bunda FM LTD, 92.1 MHz
P.O. BOX 452
BUNDA-MARA
E-mail: Ngurumoyajamii@bundafm.co.tz
PNONE NO: +255 754 279 340
+255 755 029 400
+255 717 457 216

Masafa yetu

Our major frequency is 92.1 FM, whereby we cover regions of Mara, Simiyu, Mwanza, Geita,Kagera, Shinyanga, Singida, Tabora and Katavi regions.

  • Home
  • Habari Zote
  • Kitaifa
  • Kimataifa
  • Michezo
  • Siasa
  • Uchumi na Biashara
  • About us
  • Contact
Copyright © All rights reserved. | DarkNews by AF themes.