Skip to content
March 20, 2023
  • Facebook
  • Twitter
  • Linkedin
  • Youtube
  • Instagram
Bunda FM

Bunda FM

Ngurumo ya jamii

Connect with Us

  • Facebook
  • Twitter
  • Linkedin
  • Youtube
  • Instagram

Tags

Afya Burudani Kimataifa Kitaifa Makala Michezo Muziki Siasa Uchumi na Biashara

Categories

  • Afya
  • Burudani
  • Kimataifa
  • Kitaifa
  • Makala
  • Michezo
  • Muziki
  • Siasa
  • Uchumi na Biashara
  • Home
  • Habari Zote
  • Kitaifa
  • Kimataifa
  • Michezo
  • Siasa
  • Uchumi na Biashara
  • About us
  • Contact
STAFF LOGIN
  • Home
  • MASHARTI MAPYA KWA MKONGO
  • Burudani
  • Kitaifa
  • Michezo

MASHARTI MAPYA KWA MKONGO

gasper June 7, 2022 2 min read

Yanga inaendelea na mazoezi ya kujiandaa na mechi za kumalizia msimu wa Ligi Kuu Bara pamoja na pambano lao na fainali ya michuano ya Kombe la Shirikisho la Azam (ASFC), huku kocha wao Nasreddine Nabi aliyetimkia kwao kwa mapumziko mafupi amemtumia salamu nzito mshambuliaji wake kutoka DR Congo, akimpa dili moja gumu la dakika 360.

Mshambuliaji aliyepewa masharti hayo na kutakiwa kurekebisha mambo ili mambo yamnyookee Jangwani ni Chico Ushindi, ambaye bado hajasomeka vyema kwa mashabiki tangu asajiliwe kutoka TP Mazembe kupitia dirisha dogo la usajili akipishana na Mukoko Tonombe.

Kocha Nabi alisema bado anaumizwa kichwa na Ushindi ambaye hajafanikiwa kuwasha moto walioutarajia wakati wanamchukua kwa mkopo kutoka Mazembe.

Nabi alisema katika kufanya maamuzi ya hatma ya mshambuliaji huyo anataka kumpa nafasi ya kutosha katika mechi tano zilizosalia kwa Yanga msimu huu, zikiwamo nne za Ligi Kuu na moja ya ASSFC ili kumsoma na kama atatoboa salama basi huenda akasalia kwa msimu ujao.

Ushindi alisajiliwa kwa mkataba wa miezi sita inayomalizika mwishoni mwa msimu huu, huku akiwa hajafunga bao lolote kwenye michuano hiyo ya Ligi na ASFC, lakini kocha Nabi alisema kuna vitu ameviona kwenye miguu yake katika mechi chache alizomtumia.

“Sijaanza kumjua Ushindi hapa Yanga, namjua muda mrefu lakini kuna maisha aliyapitia Mazembe ambayo yanatupa shida kuweza kuona kile alichonacho, unapomwona mazoezini ni tofauti na kwenye mechi,” alisema Nabi na kuongeza;

“Angalau mechi ya mwisho aliyocheza pale Mwanza kuna kitu kidogo alifanya, lakini kitu kibaya tunaelekea mwisho wa msimu, nafikiria kumpa hizi mechi zilizobaki kama ataweza kurudisha ubora wake.”

Nabi alisema katika mechi hizo anataka kuangalia kitu kwake kabla ya kufanya maamuzi juu ya mshambuliaji huyo kuelekea msimu ujao ambao anataka kuwa na watu wa kazi ya kweli.

Kocha huyo alisema muda mrefu amekuwa akifanya vikao vya kuwarudisha mchezoni wachezaji wake ambao wamekuwa katika hali ya kushindwa kuonyesha uwezo wao kwa kuwa bado kikosi chake kinategemea nguvu yao.

Ushindi katika muda ambao amekuwa Yanga amefanikiwa kutengeneza pasi moja pekee ya bao huku pia akishindwa kuonyesha uwezo mkubwa.

“Hapa Tanzania hakuna kitu ambacho kinaitwa kutoa muda, hiyo ni bahati mbaya sana kama akifanikiwa kujiuliza sasa tunaweza kuangalia kumpa muda kama ikiwa tofauti tutachukua maamuzi mengine.”

gasper

See author's posts

Continue Reading

Next: Simba Yaleta Mchezaji Mpya

Habari nyingine

1 min read
  • Kimataifa
  • Kitaifa

March 12, 2023
RAPA A.K.A WA AFRIKA KUSINI AMEUAWA KWA RISASI
1 min read
  • Burudani
  • Kimataifa

RAPA A.K.A WA AFRIKA KUSINI AMEUAWA KWA RISASI

February 11, 2023
NECTA Yasitisha Kutangaza Shule Bora na Mwanafunzi Bora
1 min read
  • Kitaifa

NECTA Yasitisha Kutangaza Shule Bora na Mwanafunzi Bora

January 29, 2023

RATIBA YA VIPINDI VYETU

  • 05:00 - 06:00 :- Hamka na Bunda FM
  • 06:00-06:30:- Habari za Ulimwengu (DW)
  • 06:30-07:00:- Ukurasa Mpya
  • 07:00-07:10:- Taarifa ya Habari
  • 07:10-10:00:- Ukurasa Mpya
  • 10:00-13:00:- Mchaka Mchaka
  • 13:00-14:00:- Habari za Ulimwengu (DW)
  • 14:00-16:00:- Ladha Kamili
  • 16:00-18:00:- Busati la Habari
  • 18:00-18:30:- Habari za Ulimwengu (DW)
  • 18:30-19:00:- Dance Africa
  • 19:00-19:10:- Taarifa ya Habari
  • 19:10-21:00:- Dance Africa
  • 21:00-22:00:- B-Sport
  • 22:00-01:00:- Planet Love
  • 01:00-04:00:- Usiku Mnene

  • Afya (2)
  • Burudani (5)
  • Kimataifa (6)
  • Kitaifa (16)
  • Makala (4)
  • Michezo (4)
  • Muziki (1)
  • Siasa (3)
  • Uchumi na Biashara (1)

Wasiliana nasi

Bunda FM LTD, 92.1 MHz
P.O. BOX 452
BUNDA-MARA
E-mail: Ngurumoyajamii@bundafm.co.tz
PNONE NO: +255 754 279 340
+255 755 029 400
+255 717 457 216

Masafa yetu

Our major frequency is 92.1 FM, whereby we cover regions of Mara, Simiyu, Mwanza, Geita,Kagera, Shinyanga, Singida, Tabora and Katavi regions.

  • Home
  • Habari Zote
  • Kitaifa
  • Kimataifa
  • Michezo
  • Siasa
  • Uchumi na Biashara
  • About us
  • Contact
Copyright © All rights reserved. | DarkNews by AF themes.