Skip to content
March 20, 2023
  • Facebook
  • Twitter
  • Linkedin
  • Youtube
  • Instagram
Bunda FM

Bunda FM

Ngurumo ya jamii

Connect with Us

  • Facebook
  • Twitter
  • Linkedin
  • Youtube
  • Instagram

Tags

Afya Burudani Kimataifa Kitaifa Makala Michezo Muziki Siasa Uchumi na Biashara

Categories

  • Afya
  • Burudani
  • Kimataifa
  • Kitaifa
  • Makala
  • Michezo
  • Muziki
  • Siasa
  • Uchumi na Biashara
  • Home
  • Habari Zote
  • Kitaifa
  • Kimataifa
  • Michezo
  • Siasa
  • Uchumi na Biashara
  • About us
  • Contact
STAFF LOGIN
  • Home
  • Uchumi wa Mkoa wa Mara kupaa baada ya Maonesho ya Septemba
  • Kitaifa

Uchumi wa Mkoa wa Mara kupaa baada ya Maonesho ya Septemba

Bundafm July 20, 2022 4 min read

MARA INRENATIONAL BUSINESS EXPO

 Uchumi wa Mkoa wa Mara kupaa baada ya Maonesho ya Septemba

Na Conges Mramba,Bunda FM Radio

 Kamati ya Mandalizi ya Maonesho ya Kimataifa ya Biashara mkoani Mara  imesema  Mkoa huu utarejea katika hadhi yake ya kiuchumi ya miaka ya 80 mkoa ulipokuwa na  viwanda vikubwa vya nguo, vya Maziwa,Mahoteli makubwa ya kitalii  na vinu vya kuchambulia pamba.

Wakizungumza juzi  na waandishi wa Habari, serikali na wadau  wa Biashara  wamesema, wanakusudia kupitia Maonesho Makubwa ya Biashara ya Kimataifa hapa mjini Musoma, mapema mwezi Septemba, viwanda vikubwa mithili ya Musoma Textiles(Mutex) na vingine vilivyokuwa vikichakata Maziwa, maarufu sana hapa nchini na nchi jirani kama “ Maziwa ya Mara”,vinu vya kuchambulia pamba na mazao mengine ya kimkakati,vitafufuliwa.

Aidha, Aidha, wadau hawa wanasema zamani kulikuwa na Mahoteli makubwa ya kitalii hapa mjini  Musoma  kama Hoteli iliyokuwa ikimilikiwa na Shirika la Reli(TRC) zama zile ,lakini sasa vyote havipo,na wanamatumaini baada ya maonesho haya mahoteli kama haya yatafufuliwa ili kuongeza ajira na kipato kwa wakazi wa mkoa huu.

Katibu Tawala Msaidizi anayeshughulikia Uchumi na Uzalishaji,Dk. Noel Crispine Komba, anasema viwanda vikubwa kama Mutex na vya maziwa na vile vya kuchambulia pamba vimekufa na kudumaza uchumi kwa wakazi wa mkoa huu  takriban milioni mbili,.

Mkoa huu sasa unakisiwa kuwa na  na Pato la jumla (GDP)ambalo ni takriban shilingi Bilioni tano kwa mwaka.

Dk.Komba amesema katika Mkutano na waandishi wa Habari,Julai 19 mwaka huu kwamba, matumaini ya mkoa huu ni kutumia Maonesho ya Kimataifa ya Bishara, MARA INTERNATIONAL BUSINESS EXPO, kufufua viwanda vya zamani vya Ngozi,vya maziwa,vya kusindika pamba na mafuta ya kula, na vingine vua kusindika samaki  wengi na watamu wanaopatikana ziwa Victoria ili kusisimua uchumi wa Mkoa.

“Tunakusudia viwanda na taasisi zilizokufa ama kudumaa zitapata wawekezaji na Biashara nyingine zitapata wabia wa biashara na kunyanyuka kupitia maonesho haya yanayokusudia kuleta makampuni 200 ya ndani na nje ya nchi,bila kusahau Balozi za Afrika Mashariki,Zimbabwe,Marekani na nchi za Mashariki ya Mbali”,Dk. Komba amefafanua.

Hata hivyo,Mwenyekiti wa Chama cha Wafanya Biashara,Wenye Viwanda na Kilimo)TCCIA,Mkoa wa Mara, Boniface Ndengo  alisema  Halmashauri nne za Mkoa wa Mara kati ya sita,huzungukwa na ziwa kubwa kuliko maziwa yote Barani Afrika,na ziwa la Pili Duniani kuwa na maji yasiyo na chumvi,nyuma ya ziwa la Superior lililoko Marekani,Ziwa Victoria.

Ndengo anasema, Mkoa wa Mara unatakiwa kutumia Uchumi wa Bluu kuinua uchumi wa watu “Hata Rais Samia Suluhu Hassan alipozungumza juzi alisisitiza kuhusu ‘Uchumi wa Bluu’ sasa sisi Mara tunazungukwa na ziwa hili kubwa na maarufu duniani ambalo ni nyumba ya samaki wengi watamu,na ni chanzo cha Mto maarufu Duniani,Mto Nile unaotiririka kuanzia hapa hadi hadi Bahari ya Kati”,Ndengo amefafanua.

Aidha,Mkuu huyu wa TCCIA anasema,licha ya kuwepo migodi ya madini ya dhahabu, Hifadhi na mapori tengefu,fukwe za ziwa hili,kilimo cha pamba,uvuvi,ufugaji,na kuwajirani na nchi zote za Ukanda wa Afrika Mashariki (EAC)na jumuiya ya SADC kuuza mazao anuwai yanayopatikana hapa katika masoko hayo makubwa.

“Mkoa wa Mara unapakana na Hifadhi ya Serengeti ambayo imepata tuzo ya Ubora miaka mitatu mfululizo,na asilimia 70 ya Hifadhi hii iko hapa kwetu,tunafukwe nzuri,tuna madini,kilimo cha pamba,tuna makabila zaidi ya 20 katika mkoa mmoja na kuna vivutio vingi vya kitamaduni na kitalii(Cultural Tourism),ambavyo vinaweza kufanya matajiri wakubwa wa Ukanda huu wa Afrika watoke Mara,maana kuna kila fursa na rasilimali”,amesema Ndengo.

Aidha, Mratibu Mkuu wa Maonesho haya, Bernard Mwata, amesema zaidi ya makampuni  ya biashara kubwa,za kati na Ndogo (SMEs) yaliyoalikwa katika Maonesho haya ya Kimataifa ya Mara International Business Expo, yatazalisha ajira mpya kwa vijana wanaohitimu masomo katika vyuo mbalimbali hapa nchini.

Hata hivyo,Mwata amesema wakati wa maonesho haya kutakuwa na Mashindano ya Mbio Ndefu za Riadha, Marathon kwa wanawake kwa lengo la kutangaza Hifadhi ya Serengeti.

Aidha, Mbunge wa Musoma mjini,Vedastus Manyinyi Mathayo,amesisitiza kwamba wakazi wa Mkoa wa Mara watumie Maonesho haya kukutana na wafanyabiashara wageni kuingia ubia wa kibiashara na kujifunza namna ya kutanuka kibishara ndani na nje.

The Mara International Business Expo  yataanza mapema Septemba Pili ha 11 katika viwanja vya Michezo vya Karume mjini Musoma na kumalizika Septemba 11.

Wageni takriban 100,000 wa ndani na nje ya nchi zikiwemo Balozi za mataifa ya Afrika na Mashariki ya Mbali,yamealikwa kuhudhuria maonesho haya.

Maonesho haya ambayo yana Kauli Mbiu, “BRINGING TOGETHER INVESTORS FOR FUTURE GROWTH”, yaani kuwaleta pamoja wawekezaji kwa ajili ya Maendeleo ya siku za Usoni hapa mkoani Mara,

 Sekta anuwai za biashara,Kilimo,Madini,Uvuvi,Utalii na Ujasiliamali zimealikwa kushiriki maonesho haya yanayokususdia kuwakutanisha watanzania na makapuni makubwa kadiri 500 hapa mkoani Mara.

TCCIA wa nasema  Mkoa Wa Mara unatajwa kuwa mithili ya ‘Silicon Valley’  huko Marekani mahali kuliko na dhahabu,samaki,wanyamapori wa kupendeza mashamba ya kilimo ambacho ni mali ghafi za viwanda vya bidhaa nyingi,ambapo matajiri wakubwa duniani wanaweza kutokea hapa kwenye wingi wa rasilimali.

Hata hivyo,wachambuzi wa masuala ya uchumi wamesema Mara ni mkoa ambao sasa ni Dubwana lililolala(SLEEPING GIANT)lakini linaweza kunyanyuka kupitia maonesho haya ambayo yanatazamiwa kusisimua fursa zake nyingi kama mifugo,uvuvi,kilimo cha pamba,madini,ziwa la Kihistoria,mito mikubw akama Mara unaoanzia Misitu ya Maao huko Kenya na kumwaga maji yake ziwani Victoria kilomita chache tu Kaskazini mwa mji wa Musoma,Hifadhi ya Serengeti,Makumbusho ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere yaliyoko Butiama,n.k

Bundafm

See author's posts

Continue Reading

Previous: Kesi ya Sabaya yaahirishwa tena
Next: Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Wilaya ya Bunda imevuka lengo la ukusanyaji wa mapato mwaka 2022

Habari nyingine

1 min read
  • Kimataifa
  • Kitaifa

March 12, 2023
NECTA Yasitisha Kutangaza Shule Bora na Mwanafunzi Bora
1 min read
  • Kitaifa

NECTA Yasitisha Kutangaza Shule Bora na Mwanafunzi Bora

January 29, 2023
Matokeo kidato cha nne 2022 yatangazwa, haya hapa
1 min read
  • Kitaifa

Matokeo kidato cha nne 2022 yatangazwa, haya hapa

January 29, 2023

RATIBA YA VIPINDI VYETU

  • 05:00 - 06:00 :- Hamka na Bunda FM
  • 06:00-06:30:- Habari za Ulimwengu (DW)
  • 06:30-07:00:- Ukurasa Mpya
  • 07:00-07:10:- Taarifa ya Habari
  • 07:10-10:00:- Ukurasa Mpya
  • 10:00-13:00:- Mchaka Mchaka
  • 13:00-14:00:- Habari za Ulimwengu (DW)
  • 14:00-16:00:- Ladha Kamili
  • 16:00-18:00:- Busati la Habari
  • 18:00-18:30:- Habari za Ulimwengu (DW)
  • 18:30-19:00:- Dance Africa
  • 19:00-19:10:- Taarifa ya Habari
  • 19:10-21:00:- Dance Africa
  • 21:00-22:00:- B-Sport
  • 22:00-01:00:- Planet Love
  • 01:00-04:00:- Usiku Mnene

  • Afya (2)
  • Burudani (5)
  • Kimataifa (6)
  • Kitaifa (16)
  • Makala (4)
  • Michezo (4)
  • Muziki (1)
  • Siasa (3)
  • Uchumi na Biashara (1)

Wasiliana nasi

Bunda FM LTD, 92.1 MHz
P.O. BOX 452
BUNDA-MARA
E-mail: Ngurumoyajamii@bundafm.co.tz
PNONE NO: +255 754 279 340
+255 755 029 400
+255 717 457 216

Masafa yetu

Our major frequency is 92.1 FM, whereby we cover regions of Mara, Simiyu, Mwanza, Geita,Kagera, Shinyanga, Singida, Tabora and Katavi regions.

  • Home
  • Habari Zote
  • Kitaifa
  • Kimataifa
  • Michezo
  • Siasa
  • Uchumi na Biashara
  • About us
  • Contact
Copyright © All rights reserved. | DarkNews by AF themes.